Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polepole apasua vichwa waliopita kura za maoni
Habari za Siasa

Polepole apasua vichwa waliopita kura za maoni

Humphrey Polepole, akiwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Spread the love

CHAMA cha Mapinduzi (CCM), kimeeleza kutokuwa na simile kwa wanachama wake, waliopita kwenye kura za maoni kisha kukutwa na makandokando. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho amesema, kila mwanachama aliyeshiriki ‘uovu’ katika kura za maoni, atashikishwa adabu.

Polepole ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 5 Agosti 2020, wakati akizungumza na wanahabari kwenye ofisi ndogo ya chama hicho, Lumbumba jijini Dar es Salaam.

“Muwe watulivu sababu nyie Watanzania wanawaamini kwenye wigo wa uongozi, tulieni. Hatutawaangusha watu wanyenyekevu kwenye chama chetu, muwe na amani.

“Wale mliopiga mazonge tutawafundisha adabu kipindi hiki. Sababu ukifundishwa adabu ni vizuri tukupe ‘surprise’ ukapate kazi nyingine kwa sababu uongozi unaotweza Katiba yetu hauna nafasi,” amesema Polepole.

Vikao vya Kamati za Siasa za Mkoa za CCM kuwajadili wagombea hao vilivyoanza janana vinatarajiwa kukamilika  leo Jumatano tarehe 5 Agosti 2020.

Vikao vya Kamati za Siasa za Mkoa za CCM vinafanyika baada ya mikutano mikuu ya CCM majimbo na wilaya kwa ajili ya kuchuja wagombea kufanyika.

Furaha Dominic Jacob

Mikutano mikuu ya CCM ya majimbo kwa ajili ya hatua ya awali ya kupendekeza wagombea ilifanyika Julai 20 hadi 21, 2020 ikifuatiwa na vikao vya Kamati za Siasa za Wilaya vilivyofanyika tarehe 1 hadi 2 Agosti 2020.

Hata hivyo , vikao vya Baraza Kuu la Wazazi la CCM kupendekeza wabunge viti maalum kundi la wazazi vitafanyika tarehe 9 Agosti mwaka huu, huku  Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) litafanya kura za maoni kwa wagombea wa ubunge viti maalum   tarehe 10 Agosti 2020.

Baada ya vikao hivyo kufanyika, mapendekezo yake yatawasilishwa katika vikao vya NEC.

Dk. Faustine Ndugulile

Kwa upande wa wagombea wa udiwani, tarehe 6 Agosti 2020 Vikao vya NEC ngazi ya mikoa vitafanya uteuzi wa mwisho wa wagombea wa udiwani wakata na wadi pamoja na madiwani viti maalum.

CCM kilifungua zoezi la kutafuta wagombea wake katika uchaguzi huo tarehe 14 Julai mwaka huu, ambapo watia nia katika nafasi mbalimbali walianza kuchukua siku hiyo, na kisha kurejesha fomu hizo tarehe 17 Julai 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!