Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Polepole alia na Lissu, Chadema
Habari za Siasa

Polepole alia na Lissu, Chadema

Spread the love

HUMPREY Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kukishughulikia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa madai ya kunajisi Wimbo wa Taifa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na wanahabari leo Jumatano tarehe 5 Agosti 2020 jijini Dar es Salaam, Polepole amemtaka Jaji Francis Mutingi, Msajili wa Vyama vya Siasa kuchukua hatua dhidi ya chama hicho.

Polepole amesema, angetamani kuona Msajili wa Vyama vya Siasa anazungumza lugha ya kueleweka dhidi ya tuhuma hizo.

“Ningetamani msajili azungumze lugha ya kueleweka zaidi, watu wakikosea waaambiwe na sisi tukikosea tuambiwe, Wimbo wa Taifa unaunajisi halafu unatoka unasema wapi tumevunja sheria.

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chadema

‘Wimbo huu sio wa CCM sio wa Freeman Mbowe (Mwenyekiti Chadema) na wenzake. Wimbo huu tunaimba tukiwa katikati ya vita tukiliombea Taifa,” amesema Polepole.

Aidha Polepole amekitaka Chadema kuwaomba radhi Watanzania kufuatia sakata hilo.

“Mimi nawaachia Watanzania, maana kabla hawajapewa nchi wanabadili wimbo wa Tanzania. Kabla hujaomba dhamana ya kuwa kiongozi wa nchi hii ushabadili wimbo wa Tanzania, unafanya wimbo wa chama chako.

“Mimi Watanzania naliacha hili kwenu, imetuuma sana tufanye siasa lakini tusitumie vitu vinavyogusa Watanzania vibaya bila aibu,” amesema Polepole.

Jana wakati akizungumza na wanahabari, Jaji Mutungi aliionya Chadema kutokiuka Katiba na Sheria za nchi kufuatia tuhuma hizo za kunajisi wimbo wa Taifa.

Wakati huo huo, Polepole amedai kuwa, kuna baadhi ya wanasiasa wakishirikishwa kwenye vikao vya NEC hukubali ajenda zinazoafikiwa, lakini wakitoka nje wanaeleza unafiki.

“Juzi tulikwenda kufuatilia maandalizi ya uchaguzi na yamekaa vizuri sana, tumepokea nyaraka na taarifa muhimu. Tulipewa kanuni za maadili ya uchaguzi,  sheria iko vizuri asiwadanganye mtu. Tukikaa na tume tunazungumza lugha moja wakitoka nje wanaeleza unafiki,” amesema Polepole na kuongeza:

“Tukikaa na tume tunazungumza, tunasaini nyaraka wakitoka nje wenzetu wanasema tume hii mbovu.  Huwa nawatazama. Kuna jamaa mmoja ambaye ni mbishi nasemaga huyu akitoka nje atakwenda kusema NEC si nzuri.”

Lissu aliyerejea nchini Tanzania tarehe 27 Julai 2020, akitokea Ubelgiji alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kushambuliwa na risasi mjini Dodoma mwaka 2017, aliitaka NEC kutowaengua wagombea wa vyama vya upinzani.

2 Comments

  • Mmi nashauri sheria ichukuwe mkondo kwani kiasi gani wameonesha kuwa ni chama chenye mrengo wa kihuni ambao wakipewa dhamana hawatakawia kuiuza nchi

  • Wale askari magereza walioonyeshwa wanapandisha bendera za ccm nao wahojiwe na msajili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!