Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi Mkuu: Bukoba Vijijini ‘ngoma inogile’
Habari za Siasa

Uchaguzi Mkuu: Bukoba Vijijini ‘ngoma inogile’

Conchester Rwamlaza, amechukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la Bukoba Vijijini kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

WAKATI watia nia wanane kutoka CCM katika Jimbo la Bukoba Vijijini wakichuana kuwania kuteuliwa kugombea, Conchester Rwamlaza, aliyekuwa mbunge wa Viti Maalum (Chadema) tayari amechukua fomu. Anaripoti Danson Kaijage, Bukoba…(endelea).

Rwamlaza ambaye ni mgombea mwanamke katika jimbo hilo, ametamba kushinda kwa madai, chama chake kina wanachama wengi. 

“Licha ya watia nia wengi kujitokeza kwa upande wa pili (CCM), bado mtaji wa wanachama na mashabiki wa Chadema hapa ni wengi, hili linanipa matumaini,” amesema.

Akizungumza na MwanaHALISI Online muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge, amesema sababu kuwa ni kutaka kushirikiana na wananchi kufikia ndoto ya maisha yenye mwelekeo chanya.

“Jimbo hili lina vijana ambao kimsingi wanajishughulisha lakini hawana mtetezi wa kweli. Vijana wanalima ndizi, kahawa na wengine wanajihusisha na uvuvi, lakini wamekosa mtu wa kuwaunganisha kwa kuwatafutia miundombinu ya kujikwamua,” amesema Rwamlaza.

Jimbo hilo lilikuwa likiongozwa na Jason Rweikiza (CCM) ambaye anasema, idadi kubwa ya wanaojitokeza kugombea ubunge kupitia chama hicho, itafutika baada ya jina lake kupitishwa kuwania ubunge kwa awamu nyingine.

Rweikiza ambaye amekuwa mbunge kwa vipindi kwa vipindi viwili mfululizo, anaingia kwenye wakati mgumu baada ya idadi ya wanaCCM kutaka jimbo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!