Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CUF yasaka watia nia ya urais
Habari za Siasa

CUF yasaka watia nia ya urais

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

MWISHO wa kuchukua fomu kwa ajili ya watia nia ya urais kupitia Chama cha Wananchi (CUF), sasa ni tarehe 30 Juni 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Awali chama hicho kilieleza, kuwa mwisho wa kuchukua fomu kwa watia nia ya kugombea kuteuliwa kugombea nafasi hiyo (urais) ingekuwa tarehe 16 Juni 2020, lakini mpaka juzi ni makada wawili tu waliojitokeza.

Juma Kilaghai, Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa chama hicho Taifa amesema, uamuzi wa CUF kusogeza mbele muda wa kuchukua fomu, ni kutoa fursa zaidi kwa walio na nia ya kujitokeza.

“Tumeona hakuna sababu za msingi za kutusukuma kufunga zoezi hili haraka, lakini hapa kati kulikuwa na mambo mengi na watu walikuwa na shughuli nyingi,” amesema Kilaghili.

Ofisa huyo wa CUF amesema, mpaka kufika tarehe hiyo, waliokuwa na dhamira ya kujitokeza watakuwa wamepata muda wa kutosha kujitafakari na kufanya uamuzi sahihi.

Kilaghai amesema, tayari watia nia wawili wamejitokeza kuchukua fomu, mmoja akitoka Tanzania Bara na mwingine visiwani Zanzibar.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!