Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Lwaitama: Tunapita kipindi kigumu
Habari za Siasa

Dk. Lwaitama: Tunapita kipindi kigumu

Spread the love

MWANAZUONI Dk. Azaveli Lwaitama amesema, Taifa linapita katika kipindi kigumu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020, kutokana na wananchi wengi kukata tamaa ya kushiriki kwenye uchaguzi huo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Lwaitama ambaye ni Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ametoa kauli hiyo leo Jumamosi tarehe 13 Juni 2020, wakati akihutubia mkutano ulioandaliwa na Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo aliokutana na wadau wa jimbo hilo.

Dk. Lwaitama amesema, wananchi wengi watagoma kushiriki katika uchaguzi huo, kwa hofu ya kwamba wagombea wa Chama tawala CCM, watapita bila kupingwa.

“Kipindi hiki tunapita kipindi kigumu sana. Hapa nazungumza kama mwanazuoni, kuna hatari mbele ya safari, kuna watu watajichuja wakifikiri mgombea wa CCM atapita tu bila kuchaguliwa hilo ni kusaliti uraia wako,” amesema Dk. Lwaitama.

“Haiwezekani unafikiri jimbo la ubungo tunamhitaji fulani ukarudi nyuma kisa mgombea wa chama fulani atapita. Kwa nini unakubali mambo ya ajabu,” amesema.

Dk. Lwaitama amesema nchi inapita katika kipindi kigumu kutokana na baadhi ya watu wenye hulka ya kujipendekeza, kufanya mambo ya ajabu bila kutumwa, ili wapate vyeo.

“Tutapita kipindi kigumu, kipindi hiki kuna watu wanapenda kujipendekeza watafanya vitu ambavyo hawajatumwa na mtu yeoyote, sijui ili wateuliwe?” Amehoji  Dk. Lwaitama.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!