Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yapewa somo la wagombea uchaguzi mkuu 
Habari za Siasa

Chadema yapewa somo la wagombea uchaguzi mkuu 

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Mwendeleo (Chadema) nchini Tanzania, kimepewa mbinu za ushindi kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Wabunge, Madiwani na Rais Oktoba 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Mbinu hizo zimetolewa leo Jumamosi tarehe 13 Juni 2020 jijini Dar es Salaam, na Dk. Azaveli Lwaitama, Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Dk. Lwaitama alikuwa akizungumza katika mkutano ulioitishwa na Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo kupitoa Chadema aliowakutanisha wadau wa jimbo hilo kuwaeleza mafanikio ya miaka mitano ya ubunge wake.

Mwanazuoni huyo amekishauri  chama hicho kuchagua wagombea wanaokubalika na wapiga  kura, badala ya kuchagua wagombea wanaopendwa na viongozi wa Chadema.

Dk. Lwaitama amesema, wapiga kura wengi hawana chama, hivyo wakati wanapiga kura huangalia mtu wanayemtaka na si chama cha siasa.

“Wako wengi kwenye suala hili ambao pia wengine sio wanachama wa Chadema. Kama unataka kushinda kupitia wanachama wa Chadema bado hujaelewa. Wananchi wengi hawana vyama, sababu watu wanachagua mtu hawachagui chama,” amesema Dk. Lwaitama.

Dk. Azaveli Lwaitama, Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) 

“Ukijua hilo mgombea wako atashinda na atachaguliwa na watu wa vyama mbalimbali. Mtu atachaguliwa kwa sifa zake ikiwemo kuwa karibu na wapiga kura wake,” amesema

Akisisitiza hoja yake, Dk. Lwaitama amekumbushia matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015, ambapo amesema Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), alipigiwa kura na wanachama wa CCM.

“Kuteua mgombea wa hovyo hata chaguliwa hata kama watu wanakipenda chama chako. Hata Lowassa alipigiwa kura na WanaCCM na hata wao wanajua,” amesema Dk. Lwaitama.

“Msimamishe yule ambaye wa Ubungo wanamtaka, ukimsimamisha yule Chadema anayemtaka hujaelewa. Wasikilize watu wa Ubungo wanataka nini,” Dk. Lwaitama.

Wakati huo huo, Dk. Lwaitama amewashauri wananchi kipindi cha upigaji kura, wachague mgombea bora bila kujali anatoka chama gani.

“Kwa wanachama wa vyama vingine, ujumbe wangu ni huu unapokwenda kupiga kura usifumbwe na chama angalia na mpime aliyetia nia akateuliwa na chama fulani,” amesema

Mpigie chapuo kwa sababu unaona matatizo ya jimbo lako anayabeba na hana ubaguzi sababu kama ana ubaguzi hatakusaidia sababu wananchi wa ubungo hawana chama kimoja,” amesema Dk.  Lwaitama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!