Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ndege yaanguka, 107 wahofiwa kufa
Kimataifa

Ndege yaanguka, 107 wahofiwa kufa

Spread the love

HABIRIA 107 waliokuwa ndani Airbus A320, ndege ya Shirika la Ndega la Pakistan, wanahofia kufariki dunia baada ya ndege hiyo kuangua Karachi, Pakistan ikitokea Lahore. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Sehemu ndege hiyo ilipoangukia, ilikuwa ikifuka moshi mkubwa. Ndege hiyo imenguka saa saba mchana leo tarehe 22 Mei 2020.

“Ndege yetu imeanguka Karachi. Tunajaribu kuwasiliana ili kuwa na uthibitisho idadi kamili ya watu waliokuwemo kwenye ndege hiyo.

“… lakini taarifa za awali zinaeleza, kulikuwa na abiria 99 na wahudumu wanane,” amesema Abdul Sattar Khokhar, msemaji wa mamlaka za ndege Pakistan na kuongeza “hatujawa na taarifa zaidi ya kisa hicho.”

Ndege hiyo imeanguka ikiwa ni siku chache tangu serikali ya Pakistani kuanza kuruhusi ndege za kibiashara kurejea kazini, baada ya wiki kadhaa kufungwa ili kupunguza maambukizi ya virusi vya corona.

Mpaka sasa, taarifa zaidi hazijapatikana ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!