Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Ndege yaanguka, 107 wahofiwa kufa
Kimataifa

Ndege yaanguka, 107 wahofiwa kufa

Spread the love

HABIRIA 107 waliokuwa ndani Airbus A320, ndege ya Shirika la Ndega la Pakistan, wanahofia kufariki dunia baada ya ndege hiyo kuangua Karachi, Pakistan ikitokea Lahore. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Sehemu ndege hiyo ilipoangukia, ilikuwa ikifuka moshi mkubwa. Ndege hiyo imenguka saa saba mchana leo tarehe 22 Mei 2020.

“Ndege yetu imeanguka Karachi. Tunajaribu kuwasiliana ili kuwa na uthibitisho idadi kamili ya watu waliokuwemo kwenye ndege hiyo.

“… lakini taarifa za awali zinaeleza, kulikuwa na abiria 99 na wahudumu wanane,” amesema Abdul Sattar Khokhar, msemaji wa mamlaka za ndege Pakistan na kuongeza “hatujawa na taarifa zaidi ya kisa hicho.”

Ndege hiyo imeanguka ikiwa ni siku chache tangu serikali ya Pakistani kuanza kuruhusi ndege za kibiashara kurejea kazini, baada ya wiki kadhaa kufungwa ili kupunguza maambukizi ya virusi vya corona.

Mpaka sasa, taarifa zaidi hazijapatikana ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa awali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!