Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafanyabiashara wapewa somo la kuepuka migogoro
Habari Mchanganyiko

Wafanyabiashara wapewa somo la kuepuka migogoro

Spread the love

AFISA masoko wa Jiji la Dodoma, James Yuna ameutaka Umoja wa Wafanyabiashara waendao minadani (UWABIMIDO), kufanya vikao vya mara kwa mara ili kuhakikisha wanatatua migogoro ambayo inaweza kujitokeza na kuvuruga umoja wao. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na viongozi wa Umoja wa Wafanyabiashara wa minadani mkoa wa Dodoma waliokuwa wakikutanika katika maeneo la Barabara ya kumi na moja na kuhamia maeneoya majengo ili kupisha msongamano katika barabara hiyo.

Yuna amesema wafanyabiashara hao wanatakiwa kuhakikisha wanafanya biashara zao kwa kuzingatia mazingira ambayo yanawazunguka ikiwa ni pamoja na kuondokana na migogoro.

Afisa huyo alisema kuwa wafanyabiashara wote wa minadani wanatakiwa kuwa katika eneo moja ambalo litakuwa linajulikana na kuondokana na kukaa katika maeneo ambayo yanasababisha msongamano ambao unaweza kusabaisha ajali kutokana na sehemu kuwa hatarishi.

Katika hatua nyingine Yuna alisema kuwa ili umoja huyo wa wafanyabiashara wa mnadani  uweze kudumu kunahitajika kuwepo kwa vikao vya mara kwa sambamba na kufanya maridhiano ya kweli badala ya kuishi bila kuwa na mapatano.

Pia alisema kuwa ili biashara iweze kustawi wafanyabiashara hao wanatakiwa kufanya biasha kwa njia ya utulivu,amani pamojana kuzitii mamlaka ambazo zipo kwa kufuata maelekezo wanayopewa badala ya kuwa na malumbano kwa mamlaka husika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWABIMIDO, Jeremiah Magawa alisema malengo na maazimio ya kuhamia eneo la Majengo kutoka eneo la Indipendence ni kutoka na eneo hilo kuwa dogo na kusababisha msongamano ambao haukuwa wa lazima.

Kutokana na hilo Umoja huo umeamua kutafuta eneo kubwa ambalo lipo nje ya miundombinu ya barabara na kuondoa msongamano katika eneola awali .

Hata hivyo alisema wanakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa usafiri kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kugoma kutoka eneo lenye msongamano nakuhamia katika eneo ambalo linaonekana kuwa salama.

Kutokana na hali hiyo Mwenyekiti wa umoja huo ameziomba mamlaka za Jiji la Dodoma kuhakikisha wanawaondoa wafanyabiashara waliokataa kuondoka  katika eneoambali si salama kwa wafanyabiashara hao na kusababisha msongamano usiokuwa walazima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!