Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Faini Mbowe, wenzake: 108 Mil zakusanywa usiku kucha
Habari za SiasaTangulizi

Faini Mbowe, wenzake: 108 Mil zakusanywa usiku kucha

Noti za Elfu Kumi
Spread the love

ZAIDI ya Tsh. 108,262,000 tayari zimekusanywa ndani ya saa 12, tangu faini ya Freeman Mbowe na wenzake kuwa wazi jana tarehe 10 Machi 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Fedha hizo zimekusanywa kutoka kwa wananchi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuelekea lengo la kuwakomboa viongozi hao leo tarehe 11 Machi 2020.

Taarifa iliyotolewa na Chadema leo imeeleza kuwa, mpaka kufika saa 1:20 asubuhi, kiasi hicho cha fedha tayari kimepatikana ikiwa ni pungufu ya Tsh. 246,738,000.

Nguvu ya umma kazini…hadi alfajiri ya leo Jumatano, Machi 11, 2020, mchango kupitia simu na fedha taslimu, umefikia Tsh. 108,262,000. Tunakaribia kufikia nusu. Tuendelee kuchangia na kuhamasishana kuchangia, kwa simu, benki au kutoa taslimu,” imeeleza taarifa hiyo.

Chadema kimeendelea kuhamasisha wanachama wake kuchanga TSh. 350 milioni kwa ajili ya kuwalipa dhamani viongozi wanane wa chama hicho, waliotiwa hatiani jana tarehe 10 Machi 2020 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Viongozi hao walihukumiwa kulipa kiasi hicho au kwenda jela miezi mitano kwa kila kosa. Walitiwa hatiani kwa makosa 12 kati ya 13 yaliyokuwa yanawakabili.

Hata hivyo, fedha hizo hazikupatikana jana na hivyo kupelekwa jela mpaka fedha hizo zitakapolitwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!