IKIWA zimesalia saa kadhaa kwa viongozi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuhukumiwa katika Kesi ya Jinai Na. 112/2018, inayowakabili kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wametoa waraka mzito. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).
Katika nyakati tofauti kupitia kurasa zao za Twitter, viongozi hao wametuma ujumbe wakiwataka wanachama wao kusonga mbele katika harakati za kutetea demokrasia, iwapo watakutana na hukumu ya kifungo jela.
Freeman Mbowe, Mwneyekiti wa Chadema, amesema iwapo watahukumiwa kifungo jela, wafuasi wake wasivunjike moyo.
”Tunakwenda kwenye hukumu ya kesi inayotukabili ya Mauwaji ya Akwilina,ikitokea mimi Freeman Mbowe na wenzangu tumehukumiwa kifungo Jela,naomba wanachadema popote mlipo msivunjike Moyo na wala msirudi nyuma,songeni mbele kwenye mapambano dhidi ya Udhalimu,” amesema Mbowe.
Halima Mdee, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), amewaaga rasmi wanachama wa chama hicho, akisema kwamba amejiandaa kwa lolote, akidai kwamba chochote kinaweza kutokea katika maamuzi ya kesi hiyo.
Maneno ya Halima haya hapa chini
“Wakuu salaam!! Kesho Asubuhi (leo) ni siku ya hukumu ya kesi ya viongozi wa CHADEMA na mimi nikiwa mmoja wapo.
“hochote kinaweza kutokea !!Nimewiwa kutumia nafasi hii kuwaaga rasmi. Itoshe tu kusema, binafsi nimejiandaa kiroho safi kabisa na kukubaliana na chochote kitakacho kuja.”
Leave a comment