Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Agizo la kwanza la Nondo baada ya kukwaa Uenyekiti ACT
Habari za Siasa

Agizo la kwanza la Nondo baada ya kukwaa Uenyekiti ACT

Spread the love

ABDUL Nondo, Mwanaharakati wa haki za binadamu nchini, amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ya Chama cha ACT-Wazalendo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Nondo amechaguliwa kushika wadhifa huo jana tarehe 9 Machi 2020, katika uchaguzi wa viongozi wa ngome hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya matokeo kutangazwa, Nondo aliwataka vijana wa ACT-Wazalendo kuwa wamoja kwa ajili ya kujenga chama hicho.

Wakati huo huo, Nondo  amewaomba vijana wa ACT-Wazalendo kujitokeza kwa wingi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kusikiliza hukumu ya viongozi wakuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inayotarajiwa kutolewa leo.

“Pia tunaomba vijana wote wa ACT wazalendo na viongozi  kuhudhuria na kufika Mahakama ya Kisutu leo kuanzia saa 3 asubuhi, kwani ni siku ya hukumu ya kesi dhidi ya viongozi wakuu wa chama cha Chadema,” ameagiza Nondo na kuongeza:

“Lengo ni kuonesha umoja na mshikamano kwani changamoto wanazopitia Chadema ndio changamoto ambazo viongozi wetu wa chama na chama chetu tunapitia. Hivyo naomba tujitokeze kwa wingi, pia kuzidisha maombi kwa viongozi wote wa CHADEMA, Mungu azidi kuwasimamia dhidi ya hujuma yeyote.”

Katika uchaguzi huo, Khadija Mohammed amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo Zanzibar , wakati Seleman Misango akishinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa ngome hiyo Bara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!