Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema yateua makatibu wa kanda
Habari za Siasa

Chadema yateua makatibu wa kanda

Bendera ya Chadema
Spread the love

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imeteua makatibu wa kanda sita kati ya kanda 10 za chama hicho. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 22 Februari 2020 na Tumaini Makene, Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema, uteuzi huo ulifanyika hivi karibuni katika kikao cha kamati hiyo, kilichoketi jijini Dar es Salaam, chini ya Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa chama hicho.

Makatibu walioteuliwa ni Amani Golugwa, aliyeteuliwa kuwa Katibu Kanda ya Kaskazini, General Reuben Kaduma ( Kanda ya Kusini), Ali Hemedi Mngwali (Kanda ya Pwani), Emmanuel Masonga (Kanda ya Nyasa),  Gwamaka Mbughi (Kanda ya Kati), na Kangeta Ismail Kangeta (Kanda ya Magharibi).

Taarifa hiyo imesema uteuzi wa kanda nne zilizobakia ambazo ni, Serengeti, Pemba, Unguja na Victoria, utafanywa na Kamati Kuu hapo baadae.

“Waliokuwa makatibu wa kanda waliomaliza muda wao na hawajateuliwa katika nafasi hizo, wanapangiwa majukumu mengine katika utumishi wa chama,” inaeleza taarifa ya Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!