Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba atoa masharti kuungana na Mbowe, Zitto 
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba atoa masharti kuungana na Mbowe, Zitto 

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

PROF. Ibrahim Haruna Lipumba, mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), ametoa masharti mazito ya “ushirikiano” kwa viongozi wenzake wa vyama vya ACT- Wazalendo na Chama cha Demokarsia (Chadema), kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari, leo Jumatatu, makao makuu ya chama chake, Buguruni, Prof. Lipumba amesema, ili CUF iungane na Chadema na ACT- Wazalendo, ni sharti vyama hivyo, “visipokee mabaki” kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM). 

Amesema, “nipo tayari kuungana na Mbowe na Zitto Kabwe, pamoja na vyama vingine vya upinzani, iwapo watakuwa tayari kutekeleza sharti hilo. Vinginevyo, sisi kama CUF tutakwenda kivyetu na wao kivyao.”

Kwa mujibu wa Prof. Lipumba, CUF haiko tayari kuungana na vyama vinavyosubiria wagombea walioenguliwa na kuonekana hawafai katika nafasi mbalimbali ndani ya CCM.

Kiongozi huyo wa CUF ametoa msimamo huo, kufuatia kauli ya Zitto, kwamba vyama vya upinzani havina budi kuungana katika uchaguzi huo, ili viking’oe chama tawala madarakani.

Kupitia mkutano huo, Prof. Lipumba amesema vyama vya upinzania mpaka sasa havijazungumza chochote kuhusu ushirikiano huo.

“Huwezi sema ushirikiano wakati hujaongea na vyama. Unatakiwa ushirikiano wa kuitoa CCM madarakani na sio ushirikiano wa kusubiri mabaki ya CCM.

“Sio utaratibu wa kufanya umoja wa kusubiri nani atakeyetemwa na CCM au kuenguliwa. Tutashirikiana na vyama vyenye nia ya dhati ya kusimamia mabadiliko ya kweli,” ameeleza Prof. Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!