Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba atoa masharti kuungana na Mbowe, Zitto 
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba atoa masharti kuungana na Mbowe, Zitto 

Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF
Spread the love

PROF. Ibrahim Haruna Lipumba, mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), ametoa masharti mazito ya “ushirikiano” kwa viongozi wenzake wa vyama vya ACT- Wazalendo na Chama cha Demokarsia (Chadema), kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari, leo Jumatatu, makao makuu ya chama chake, Buguruni, Prof. Lipumba amesema, ili CUF iungane na Chadema na ACT- Wazalendo, ni sharti vyama hivyo, “visipokee mabaki” kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM). 

Amesema, “nipo tayari kuungana na Mbowe na Zitto Kabwe, pamoja na vyama vingine vya upinzani, iwapo watakuwa tayari kutekeleza sharti hilo. Vinginevyo, sisi kama CUF tutakwenda kivyetu na wao kivyao.”

Kwa mujibu wa Prof. Lipumba, CUF haiko tayari kuungana na vyama vinavyosubiria wagombea walioenguliwa na kuonekana hawafai katika nafasi mbalimbali ndani ya CCM.

Kiongozi huyo wa CUF ametoa msimamo huo, kufuatia kauli ya Zitto, kwamba vyama vya upinzani havina budi kuungana katika uchaguzi huo, ili viking’oe chama tawala madarakani.

Kupitia mkutano huo, Prof. Lipumba amesema vyama vya upinzania mpaka sasa havijazungumza chochote kuhusu ushirikiano huo.

“Huwezi sema ushirikiano wakati hujaongea na vyama. Unatakiwa ushirikiano wa kuitoa CCM madarakani na sio ushirikiano wa kusubiri mabaki ya CCM.

“Sio utaratibu wa kufanya umoja wa kusubiri nani atakeyetemwa na CCM au kuenguliwa. Tutashirikiana na vyama vyenye nia ya dhati ya kusimamia mabadiliko ya kweli,” ameeleza Prof. Lipumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mobhare Matinyi Msemaji mpya wa Serikali

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa Mkuu wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar

Spread the loveBasi  Jeshi la Magereza lenye namba MT 0040 limegonga treni...

error: Content is protected !!