Saturday , 2 December 2023
Habari za Siasa

Sumaye arudi CCM

Spread the love

FREDERICK Sumaye, Waziri Mkuu wa zamani amerejea katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), leo tarehe 10 Februari 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Sumaye ametangaza kurejea akiwa kwenye ofisi ndogo ya chama hicho Mtaa wa Lumumba, jijini Dar es Salaam ambapo amepokewa na Dk Bashiru Ally, katibu mkuu wa chama hicho.

Sumaye aliyehuduma kama Waziri Mkuu kwa miaka 10 katika serikali ya Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ametangaza kurejea CCM kwenye kikao cha ndani cha chama hicho kilichokuwa kikiendelea leo.

Hatua ya Sumaye kuhamia CCM imetanguliwa na kujivua uanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), zaidi ya miezi miwili iliyopita.

Alijivua uanachama Chadema kwa kile alichokiita ‘figisu’ kwenye uchaguzi wa Uenyekiti wa Kanda ya Pwani Chadema, ambapo licha ya kuwa mgombea pekee, lakini alipigiwa kura nyingi za hapana.

Tarehe 22 Agosti 2015, Sumaye alijiengua CCM na kuhamia Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia kuzindua programu ya nishati safi ya kupikia kwa wanawake Afrika

Spread the loveRais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua programu ya...

Habari za Siasa

AG aiagiza kamati ya maadili kuwashughulikia mawakili wanaokiuka maadili

Spread the loveMWANASHERIA Mkuu wa Serikali (AG), Dk. Eliezer Feleshi, ameagiza Kamati...

Habari za Siasa

Jaji avunja ukimya sakata la Mpoki kusimamishwa uwakili

Spread the loveJAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amekitaka Chama cha...

Habari za Siasa

Sheikh Ponda ataka mwarobaini changamoto uchaguzi 2020

Spread the loveKATIBU Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa...

error: Content is protected !!