Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wapinzani kujitoa uchaguzi serikali za mitaa, kwaitesa CCM
Habari za SiasaTangulizi

Wapinzani kujitoa uchaguzi serikali za mitaa, kwaitesa CCM

Humphrey Polepole, Aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Spread the love

HATUA ya vyama nane vya upinzani kujitoa katika kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2019, ilishtua Chama cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 18 Januari 2020 na Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, wakati akizungumza katika darasa la itikadi kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, jijini Dar es Salaam.

Polepole amesema CCM ilipata mshtuko kwa kuwa, haikutegemea kama vyama hivyo vya upinzani vingechukua hatua hiyo.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi CCM amesema, chama chake kilijipanga kufanya kampeni kwa ajili ya kuchuana katika uchaguzi huo.

“Walipojitoa tumebaki CCM, tulikuwa tunawasubiri, tumejipanga kupiga kampeni hatari lakini wamejitoa wote. Tumepata mshutuko sababu nilikuwa najua nitapiga hapa, nitapiga kule lakini hakuna,” ameeleza Polepole.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ACT-Wazalendo, Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), ni miongoni mwa vyama nane vilivyosusia uchaguzi huo uliofanyika tarehe 24 Novemba 2019, kwa maelezo kwamba mchakato wake ulikuwa unapendelea wagombea wa CCM.

Katika uchaguzi huo, CCM ilishinda kwa asilimia 99.9 baada ya wagombea wake katika nafasi za uenyekiti wa kijiji, serikali za mitaa na kitongoji kupita bila kupingwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!