Wednesday , 8 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Pakistan ahukumiwa kifo
Kimataifa

Rais Pakistan ahukumiwa kifo

Perves Musharraf
Spread the love

PERVES Musharraf, aliyekuwa Rais wa Pakistan (76) amehukumiwa adhabu ya kifo, baada ya kukutwa na hatia ya kosa la uhaini. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hukumu hiyo imetolewa leo tarehe 16 Desemba 2019, na Jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Juu ya Pakistan, huku rais huyo mstaafu akiwa hayupo mahakamani hapo.

Jopo hilo la majaji watatu lilimkuta Musharraf na hatia, kwenye kosa la uhaini pamoja na kuvunja katiba ya nchi hiyo, akiwa madarakani.

Mahakama hiyo imeamuru Musharraf anayeishi uhamishoni, Dubai katika Nchi za Falme za Kiarabu, akamatwe, kama atagoma kurudi nchini Pakistan.

Musharraf amekutwa na hatia kwa kosa la kusitisha matumizi ya katiba ya Pakistan na kuanzisha sheria ya dharula, mwaka 2007.

Makosa mengine yaliyokuwa yana mkabili Musharraf,  ni mauaji ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Pakistan, Benazir Bhutto, aliyeuawa mwaka 2007 katika shambulio la kujitoa mhanga na mauaji ya halaiki ya watu.

Musharraf kwa mara ya kwanza alifikishwa kortini kwa tuhuma za uhaini, mwezi Desemba mwaka 2013, na kushtakiwa rasmi tarehe 31 Machi 2014.

Musharraf aliingia madarakani kwa mapinduzi mwaka 1999, ambapo alitawala kwa miaka 9, baada ya kujiuzulu urais wa Pakistan mwaka 2008, akikwepa kufunguliwa kesi kuhusu tuhuma zilizokuwa zinamkabili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!