Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mvua yachafua hali ya hewa, DART yasitisha usafiri
Habari Mchanganyiko

Mvua yachafua hali ya hewa, DART yasitisha usafiri

Spread the love

MVUA iliyoanza kunyesha mfululizo kuanzia alfajiri ya leo tarehe 17 Desemba 2019, imeleta adha kwa wakazi Jiji la Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mvua hiyo imesababisha nyumba zilizoko mabondeni kujaa maji na barabara kutopitika, hali iliyopelekea baadhi ya wananchi kukwama kuendelea na shughuli zao za kijamii.

Miongoni mwa maeneo hususan kwenye barabara, yaliyoathiriwa na mvua hiyo ni pamoja na barabara ya Morogoro maeneo ya Jangwani,  baadhi ya sehemu katika Barabara ya Mandela.

Na barabara ya Shekilango maeneo ya daraja la Mugabe, barabara ya Kawawa maeneo ya Kinondoni Mkwajuni.

Kufuatia adha hiyo, Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART),  imesitisha safari zake kutoka Kimara na Morocco kuelekea Kivukoni, Kariakoo na Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa ya wakala huo iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa twitter, wasafiri wanashauriwa kutumia usafiri mbadala ili kufika maeneo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!