Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msajili aionya Chadema, Prof. Safari aduwaa
Habari za SiasaTangulizi

Msajili aionya Chadema, Prof. Safari aduwaa

Profesa Abdallah Safari,makamu mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

HATUA ya Frederick Sumaye, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Kanda ya Pwani kuangushwa kwenye uchaguzi wa kanda hiyo, imemshtua Prof. Abdallah Safari, makamu mwenyekiti wa chama hicho. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Wakati mvumo wa mizengwe kutumika kumwangusha Sumaye ukishika kasi, Ofisi ya Msaji wa Vyama vya Siasa imeonya, kwamba kuna hatari ya viongozi wa juu kutotambuliwa na ofisi hiyo, iwapo itajiridhisha kanuni za uchaguzi huo zimebakwa.

Uchaguzi wa ndani wa chama hicho katika ngazi mbalimbali unaendelea nchini, ambapo tamati ya uchaguzi huo inatarajiwa kuwa tarehe 18 Desemba 2019, pale viongozi wakuu wa chama hicho watakapopatikana.

Prof. Safari akizungumza na mtandao huu, ameonesha kushangazwa baada ya Sumaye kuangushwa kwenye uchaguzi huo uliofanyika tarehe 28 Novemba 2019.

“Ninavyomjua Sumaye na jinsi alivyo lulu kwenye chama hiki, Chadema kimepoteza lulu kwenye kanda hiyo. Sumaye ni muungwana, mwadilifu na mwenye uwezo mkubwa kwenye uongozi.

“Nawatahadharisha Chadema pia nawaonya kwamba wanacheza na lulu. Naona wanazungumzia demokrasia lakini nashangaa kwanini hawawajui watu wenye weledi, uwezo mkubwa na mawazo chanya katika kuongoza. Sielewi kwanini hili halionekani ndani ya chama,” amesema Prof. Safari.

Prof. Safari ambaye ni mwanasheria mkongwe amesema, anatarajia kuendelea na maisha yake baada ya kukabidhi nafasi yake ya umakamu mwenyekiti kwa viongozi wajao.

Sisty Nyahoza, Naibu Msajili katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, ametahadharisha Chadema kuzingatia kanuni za uchaguzi.

Akizungumza na chombo kimoja cha habari nchini, Nyahoza kwa niaba ya msajili wa vyama amesema, ofisi yake haitaona tabu kutotambua viongozi watakaochaguliwa pale itapojiridhisha kama mbinu hasi zilitumika.

Tarehe 18 Novemba 2019, chama hicho pamoja na mambo mengine, kinatarajiwa kupata viongozi wake wakuu akiwemo mwenyekiti Taifa.

Hata hivyo, unapofika katika kuwania uenyekiti wa chama hicho mwaka 2004, demokrasia huyumba na kumfanya Mbowe aendelee kuwa mwenyekiti.

Waliowahi kujitokeza kuchuana na Mbowe akiwemo Chacha Wange na Zitto Kabwe, waliishia njiani. Kwenye kinyang’anyiro cha sasa, Mbowe atavaana na Sumaye pia Cecil Mwambe (Mbunge wa Ndanda).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

error: Content is protected !!