Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli afanya uteuzi, atengua
Habari za Siasa

Rais Magufuli afanya uteuzi, atengua

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli leo tarehe 19 Oktoba 2019 amefanya uteuzi na utenguzi wa viongozi mbalimbali. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Rais Magufuli amemteua Mathias Kabunduguru kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania. 

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, Kabunduguru aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia elimu, anachukua nafasi ya Hussein Katanga ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Pia, Rais Magufuli amemteua Godfrey Mweli, kuwa Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia elimu. Kabla ya uteuzi huo, Mweli alikuwa Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Sheria na Katiba.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Hashim Komba, kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea akichukua nafasi ya Rukia Muwango ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Hali kadhalika, Rais Magufuli amemteua Hassan Rungwa, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!