Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Uongozi unahitaji uvumilivu
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Uongozi unahitaji uvumilivu

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema, kazi ya uongozi inahitaji uvumilivu pamoja na kumtanguliza Mungu katika kila jambo. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo tarehe 20 Oktoba 2019, Ikulu jijini Dar es Salaam katika hafla ya uapisho wa viongozi mbalimbali,aliowateua jana.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, amesema wakati mwingine kazi ya uongozi ni kuchafuliwa badala ya kusemwa kwa mazuri.

“Saa nyingine katika uongozi inahitaji uvumilivu, kumtanguliza Mungu mbele. Utasemwa saa nyingine, usisemwe vizuri. Lakini hiyo ndiyo kazi ya uongozi. Kazi ya uongozi saa nyingine ni kuchafuliwa,” amesema Rais Magufuli.

Kauli hiyo ya Rais Magufuli imekuja katika kipindi ambacho kuna sintofahamu, kufuatia baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii, kumzushia ugonjwa na hata wengine kudai kwamba ameaga dunia.

Kuhusu viongozi aliowaapisha, Rais Magufuli amewataka kuzingatia maadili, sheria na haki katika utekelezaji wa majukumu yao.

Miongoni mwa viongozi walioapishwa ni, Mathias Kabunduguru, aliyeteuliwa kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Kabunduguru aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia elimu, anachukua nafasi ya Hussein Katanga ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Pia, Godfrey Mweli aliyeapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia elimu. Awali, Mweli alikuwa Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Sheria na Katiba.

Kipngozi mwingine aliyeapishwa na Rais Magufuli ni Hashim Komba,Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea akichukua nafasi ya Rukia Muwango ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Hali kadhalika, Hassan Rungwa, ameapishwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!