Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mama Samia kumwakilisha JPM uzinduzi wa mkutano wa AALCO
Habari za Siasa

Mama Samia kumwakilisha JPM uzinduzi wa mkutano wa AALCO

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

MAMA Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, anatarajia kumwakilisha Rais John Magufuli kwenye uzinduzi wa mkutano wa 58 wa Shirika la Mashauriano ya Kisheria ya Nchi za Asia na Afrika (AALCO). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Hayo amesema Dk. Augustine Mahiga, Waziri wa Katiba na Sheria leo tarehe 19 Oktoba 2019, wakati akizungumza na wanahabari kuhusu mkutano huo unaoafanyika kwa muda wa siku tano, kuanzia tarehe 21 hadi 25 Oktoba mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Dk. Mahiga amesema Mama Samia ataufungua mkutano huo kwa niaba ya Rais Magufuli, siku ya Jumatatu tarehe 21 Oktoba 2019.

“Mgeni rasmi katika mkutano huu atakuwa Mheshimiwa Mama Samia, kwa niaba ya Rais Magufuli,” amesema Dk. Mahiga.

Dk. Mahiga ameeleza kuwa, washiriki wa mkutano huo ni mawaziri wa shera, wanasheria wakuu pamoja na mabalozi wa nchi 48 kutoka barani Asia na Afrika, ambazo ni mwanachama wa AALCO.

“Washiriki ni mawaziri wa sheria na wanasheria wakuu. Na hapa Tanzania utafunguliwa na Makamu wa Rais, Mama Samia,” amesema Dk. Mahiga.

Dk. Mahiga amesema washiriki wa mkutano huo watajadili masuala mbalimbali kuhusu sheria za kimataifa na changamoto zake.

“Umoja huu ulijikita katika sekta ya sheria. Huu mkutano ambao unafanyika kila mwaka,  Unajishughulisha na masuala ya kisheria katika jumuiya ya kimataifa.  Kuna masuala mengi na changamoto nyingi ambapo nchi moja haiwezi kutatua,” amesema Dk. Mahiga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!