Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uhujumu uchumi: Kigogo mwingine ajitosa kwa DPP
Habari za Siasa

Uhujumu uchumi: Kigogo mwingine ajitosa kwa DPP

Kuluthum Mansoor, akiwa mahakamani wakati wa kesi yake
Spread the love

KULUTHUM Mansoor, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), amekiri kosa na kutaka yaishe. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Elia Mwingira, Wakili wa Utetezi ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwamba wameandika barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Makosa nchini (DPP) Biswalo Mganga kukiri makosa ya Kuluthum.

Kigogo huyo wa Takukuru anakabiliwa na mashtaka manane likiwemo la utakatishaji fedha kiasi cha Sh. 477 Bil. Mashitaka mengine ni kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Wakili wa Kuluthum ametoa kauli hiyo baada ya Wankyo Simon, wakili wa serikali mwandamizi kudai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika.

Hata hivyo, wakili Mwingira ameiomba mahakama kuzingatia kwamba, mteja wake tayari ameandika barua hiyo kwa lengo la kutaka apatiwe haki yake ya msingi.

Pamoja na maelezo hayo, Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina ameahirisha shauri hilo mpaka tarehe 16 Oktoba 2019 itakapotajwa tena.

Jumapili ya tarehe 22 Septemba 2019, Rais John Magufuli alishauri ofisi ya DPP, kwamba wale wenye kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, kama wapo tayari kuomba radhi na kurejesha fedha, ofisi hiyo iangalie utaratibu wa kuwaachia ndani ya siku saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!