KULUTHUM Mansoor, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), amekiri kosa na kutaka yaishe. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Elia Mwingira, Wakili wa Utetezi ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwamba wameandika barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Makosa nchini (DPP) Biswalo Mganga kukiri makosa ya Kuluthum.
Kigogo huyo wa Takukuru anakabiliwa na mashtaka manane likiwemo la utakatishaji fedha kiasi cha Sh. 477 Bil. Mashitaka mengine ni kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
Wakili wa Kuluthum ametoa kauli hiyo baada ya Wankyo Simon, wakili wa serikali mwandamizi kudai mahakamani hapo kuwa, upelelezi haujakamilika.
Hata hivyo, wakili Mwingira ameiomba mahakama kuzingatia kwamba, mteja wake tayari ameandika barua hiyo kwa lengo la kutaka apatiwe haki yake ya msingi.
Pamoja na maelezo hayo, Hakimu Mfawidhi, Kelvin Mhina ameahirisha shauri hilo mpaka tarehe 16 Oktoba 2019 itakapotajwa tena.
Jumapili ya tarehe 22 Septemba 2019, Rais John Magufuli alishauri ofisi ya DPP, kwamba wale wenye kesi za uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, kama wapo tayari kuomba radhi na kurejesha fedha, ofisi hiyo iangalie utaratibu wa kuwaachia ndani ya siku saba.
Leave a comment