SERIKALI imeeleza, bado inadaiwa kiasi cha Sh. 50 bilioni na wakulima wa zao za korosho. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Akizungumza na wanahabari leo tarehe 20 Septemba 2019, Japhet Hasunga, Waziri wa Kilimo amesema serikali ilikuwa inadaiwa zaidi ya Sh. 720 bilioni na kwamba imelipa na kusalia 50 bilioni.
“Serikali ilikuwa inadaiwa zaidi ya Sh. 720 bilioni na wakulima wa korosho, mpaka sasa bado tunadaiwa Sh. 50 bilioni. Bado malipo yanaendelea, hivi ninavyoongea inawezekana deni limepungua.
“Tunauza korosho na hela zinazopatikana tunalipa wakulima hela yao kwanza. Kipaumbele chetu ni kuhakikisha mkulima analipwa ili apate fedha za kuandaa mashamba,” amesema Hasunga.
Hasunga ameeleza kwamba, serikali itawalipa wakulima fedha zao zote kabla ya msimu mpya wa korosho haujaanza.
Amesema hadi sasa kuna kampuni takribani 15 zinanunua korosho hizo, na kuwa serikali ikipata fedha itawalipa kwanza wakulima.
Korosho zilikuwepo tani 2240000 kati ya hizo 2129 ziliuzea katika mnada wa awali, zile 222000 kiasi tumebangua ndani zingine tunaendelea kuuza.
“Kuhusu biashara ya sasa hivi inayoendelea ni kweli mimi nimesikia kwamba zote zimeuzwa lakini kwa mujibu wa mkataba wa makubaliano kuna kampuni kama 15 zinazonunua korosho na kila kampuni utaratibu wake ni kwamba mzigo ukiingia kwenye meli zinafanya malipo.
Ni sh ngapi kuna kamati maalumu inayosimamia zoezi la uuzaji pia tuna wizara ya viwanda na biashara ndio kazi yao. Mimi kazi yangu ni kusimamia uzalishaji na ukusanyaji na nishaimaliza.”
Leave a comment