Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Si akili zao, ni kufilisika
Habari za SiasaTangulizi

Si akili zao, ni kufilisika

Spread the love

KUFILISIKA huwa hakupigi goti. Wala anayefilisika huwa hajijui; huwa anadhani kilichopungua leo atafidia kesho. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Mfano, mfanyabiashara wa duka, kwa kawaida hupanga bidhaa zake kwenye shelfu. Bidhaa zikianza kupungua tu, ili kuonesha bado zimejaa hupanga maboksi, na kadri anavyozidi kufilisika, hata maboksi hukosekana, shelfu zinabaki wazi.

Hata kufilisika kisiasa hakupigi hodi. Mwanasiasa akifilisika hupanga maboksi akilini mwake. Hebu kitazame Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilivyo na watu maarufu na wasomi lukuki, angalia mijadala yao – wao kwa wao wanatuhumiana, wanatukanana- huku ndio kufilisika.

Hizi sio akili zao! Chama tawala kinafurahia matusi? Wanamtunza mtu anayetukana? Tena wanatukana wazee, watoto wadogo wanapaza sauti, wanawatukani.

Ila kwa uamsho huu wa bongo mpya za vijana na mitandao ya kijamii, hawaponi. Wanaojua kukokotoa wanaweka hesabu hadharani, kuhoji kwao kunafungua masikio wananchi. Siku hazigandi, 2020 hiyo hapo.

Kama muuza duka vile, watu wanaofilisika hawajijui. Kinachowatia upofu ni mamlaka zao, wanaamini kwamba wanaweza kulazimisha mahaba kwa hadaa. Never, nasema never.

Unawezaje kuwajua watu aliyefilisika? Hujengwa na hulka kadhaa, miongoni mwao ni zile zinazowaingiza katika kundi la upofu. Huziba mishipa ya fahamu huku wasiruhusu bongo zao kutawala mifumo yao ya fahamu.

Hawa huamini kuwa, ‘kelele’ za wasiowapenda zinapaswa kuzimwa bila kujali wanapanda mbegu gani, kinachowatosha wao ni ‘uungu’ katika uso wa dunia. Hizo ndio akili zao.

Wamefunika historia kwamba, wakoloni hawakuondoka kwa mahaba na waafrika, kilichowasukuma kufanya hivyo ni muda.

Tukumbushane kwamba hakuna aliye salama katika mazingira yanayotawaliwa na utesaji, utekani na upotezwaji, kila mwenye nafasi anapaswa kupinga na kukemea.

Tukumbushane kuwatekwa, kuteswa na kupotezwa ni mambo tusiyoyataka na hayavumiliki. Jukumu la kuzuia haya ni la kila mmoja wetu. Wakati ni sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!