Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waliojitokeza kumrithi Lissu hawa hapa
Habari za SiasaTangulizi

Waliojitokeza kumrithi Lissu hawa hapa

Tundu Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

WAGOMBEA kutoka vyama 12 vya siasa nchini, wamejitokeza kuchukua fomu ya kuwania ubunge katika Jimbo la Singida Mashariki. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ni baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutangaza tariba kuanza kuchukua fomu, kurejesha, kuanza kampeni na mwisho wa kampeni na kisha kufanya uchaguzi tarehe 31 Julai 2019.

Chama cha Wananchi (CUF), kimemsimamisha Selemani Ntandu, Masalio Kyara (SAU), Amina Mcheka (AAF), Donald Mwanga (TLP) na Hamidu Hussein (ADA-Tadea).

Wengine ni Ayuni John (UDP), Feruzy Fenezyson (NRA), Maulid Mustafa (ADC), Ameni Npondia (CCK), Abdallah Tumbo (UMD), Amina Ramadhan (DP), Tirubya Mwanga (UPDP).

Mpaka sasa, Miraji Mtaturu ambaye ndio mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hajajitokeza kuchukua fomu.

Jimbo la Singida Mashariki linatarajiwa kuingia kwenye uchaguzi mdogo baada ya Job Ndugai, Spika wa Bunge kutengua ubunge wa Tundu Lissu kwa madai ya utoro na kushindwa kujaza fomu ya maadili.

Lissu ambaye ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, yupo nje ya nchi kwa matibabu baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi tarehe 7 Septemba 2017.

Shambulio hilo lilitokea mchana nyumbani kwake Area D, jijini Dodoma muda mfupi baada ya kutoka kwenye vikao vya Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!