Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM aipa Wizara ya Fedha, Ujenzi siku 5
Habari za Siasa

JPM aipa Wizara ya Fedha, Ujenzi siku 5

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli ametoa siku tano kwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Wizara ya Fedha na Mipango, kuhakikisha vifaa vya ujenzi wa chelezo ya kujengea meli vilivyokwama bandari ya Dar es Salaam kwa sababu ya kodi, vinaachiliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo alipotembelea Bandari ya Mwanza, kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa chelezo, ukarabati wa meli 5 na ujenzi wa meli mpya katika Ziwa Victoria, unaogharimu zaidi ya Sh. 150 Bilioni, unaofanywa na kampuni 2 kutoka nchi ya Jamhuri ya Korea.

Rais Magufuli ameagiza wizara ya fedha iliyo chini ya Dk. Phillip Mpango na Wizara ya ujenzi iliyo chini ya Isack  Kamwelwe, kuhakikisha vifaa hivyo, ikiwemo na vifaa vya ukarabati wa meli, vilivyokwama kutokana na mchakato wa kikodi vinafikishwa katika Bandari ya Mwanza.

Aidha, Rais Magufuli amekasirishwa na ucheleweshwaji wa makontena 58 yenye vifaa vya ujenzi vilivyoagizwa na kampuni ya ukandarasi za Korea Total Marine Innovation (KTMI) na STK JV Saekyung Construction Ltd za Korea, kwa kusubiri msamaha wa kodi.

Wakati huo huo, Rais Magufuli ameagiza mitambo miwili ya kunyanyulia mizigo iliyokuwa imeuzwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) kurejeshwa mara moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!