Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waliojitokeza kumrithi Lissu hawa hapa
Habari za SiasaTangulizi

Waliojitokeza kumrithi Lissu hawa hapa

Tundu Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

WAGOMBEA kutoka vyama 12 vya siasa nchini, wamejitokeza kuchukua fomu ya kuwania ubunge katika Jimbo la Singida Mashariki. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Ni baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutangaza tariba kuanza kuchukua fomu, kurejesha, kuanza kampeni na mwisho wa kampeni na kisha kufanya uchaguzi tarehe 31 Julai 2019.

Chama cha Wananchi (CUF), kimemsimamisha Selemani Ntandu, Masalio Kyara (SAU), Amina Mcheka (AAF), Donald Mwanga (TLP) na Hamidu Hussein (ADA-Tadea).

Wengine ni Ayuni John (UDP), Feruzy Fenezyson (NRA), Maulid Mustafa (ADC), Ameni Npondia (CCK), Abdallah Tumbo (UMD), Amina Ramadhan (DP), Tirubya Mwanga (UPDP).

Mpaka sasa, Miraji Mtaturu ambaye ndio mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), hajajitokeza kuchukua fomu.

Jimbo la Singida Mashariki linatarajiwa kuingia kwenye uchaguzi mdogo baada ya Job Ndugai, Spika wa Bunge kutengua ubunge wa Tundu Lissu kwa madai ya utoro na kushindwa kujaza fomu ya maadili.

Lissu ambaye ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, yupo nje ya nchi kwa matibabu baada ya kushambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi tarehe 7 Septemba 2017.

Shambulio hilo lilitokea mchana nyumbani kwake Area D, jijini Dodoma muda mfupi baada ya kutoka kwenye vikao vya Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!