Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee Chadema ‘wabisha hodi’ kwa Spika Ndugai, Rais Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Wazee Chadema ‘wabisha hodi’ kwa Spika Ndugai, Rais Magufuli

Spread the love

BARAZA la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameeleza wasiwasi kuhusu gharama za matibabu ya Job Ndugai, Spika wa Bunge nchini India na mkataba wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kutokana na wasiwasi huo, wameitaka serikali kuwasilisha bungeni ripoti ya matibabu ya Spika Ndugai na mkataba wa SGR bungeni ili kupitiwa.

Wito huo umetolewa leo tarehe 5 Julai 2019 na Hashimu Juma, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Chadema wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Juma ameeleza kuwa, baraza hilo lina wasiwasi kufuatia mradi wa SGR kutekelezwa pasipo kupitishwa na Bunge.

“Tunataka mikataba ya mradi wa Standard Gauge aliyosema Rais John Magufuli anatengeneza reli kutoka Dar es Salaam mpaka wapi sijui….,” amesema Juma.

Kuhusu ripoti ya matibabu ya Spika Ndugai, Juma amesema ni vyema serikali ikaiwasilisha bungeni ili kuueleza umma aina ya matibabu aliyopatiwa pamoja na ghama zake.

“Wakati serikali imeanza, Ndugai alikwenda kutibiwa India, matokeo yake aliporudi alisema katumia dola 12 milioni. Maradhi gani hayo, kafanya operesheni ngapi, kaenda hospitali gani?  hakuna, huo ni ufisadi.  Hiyo ilikuwa njia ya kuvusha kodi za Watanzania.

“Huo ni ufisadi wa kutisha, tunataka tuone ripoti zote zirudishwe, ziwasilishwe bungeni. Tunataka vyeti vya hoispitali, hesabu za madaktari na kafanya upasuaji ngapi,” amesema Juma.

Pia mwenyekiti huyo amesema, baraza hilo limeshauri serikali kuwafikisha katika Mahakama ya mafisadi, Spika Ndugai na wabunge wa CCM kwa madai ya kupitisha azimio la kutofanya kazi na Profesa Mussa Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Juma amesema, baraza hilo limetoa wito huo kutokana kwamba spika na wabunge hao wanakiuka katiba na sheria za nchi, kwa kukataa kufanya kazi na mtu anayesimamia hesabu za serikali.

“Kama kweli umedhamiria kufungua mahakama ya ufisadi, fisadi..  mchukue Spika Ndugai na wabunge wote wa CCM waliokataa kufanya kazi na CAG,” amesema Juma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!