Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai ‘afyeka’ hotuba ya upinzani
Habari za Siasa

Spika Ndugai ‘afyeka’ hotuba ya upinzani

Job Ndugai, aliyekuwa Spika wa Bunge Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri, amefyeka baadhi ya vipengele vilivyokuwa ndani ya Hotuba ya Waziri Kivuli wa Wizara ya Fedha na Mipango kwa Mwaka wa Fedha 2019/20. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Taarifa ya kufyekwa kwa vipengele hivyo imetolewa na Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika akieleza kuwa, Spika Ndugai alitoa maagizo ya kufutwa baadhi ya vipengele na maneno.

Akitoa maelezo hayo leo tarehe 17 Juni 2019, bungeni jijini Dodoma Dk. Ackson amesema kuwa, vipengele vilivyoondolewa katika hotuba hiyo vinatoka katika aya ya 18, 30, 31, 43, 44, 45, 46, 47, 48 49, 50 na 52.

Pia, katika hotuba hiyo kimeondolewa kipengele A chote, I-J aya 104 hadi 110, sehemu A yote aya ya 118 hadi 135, sehemu O aya 147 hadi 148 na sehemu Q yote aya ya 152 hadi 157.

Hotuba hiyo imesomwa leo  na David Silinde, Naibu Waziri Kivuli wa Fedha na Mipango ambapo ameeleza kulalamika hatua ya kufutwa vipengele hivyo bila kupewa taarifa.

Akitoa malalamiko hayo Silinde ameshauri kuwa, ni vema sasa pale kiti cha spika kinapofanya maamuzi, kiwe kinatoa taarifa mapema tofauti na ilivyo sasa.

Hotuba hiyo iliyosomwa leo, ilipaswa kusomwa siku ya bajeti kuu, tarehe 13 Juni 2019, hata hivyo haikusomwa kutokana na kuwa na saini ya Halima Mdee, Waziri Kivuli wa Fedha ambaye anatumikia adhabu ya Bunge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!