Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ‘aichoka’ TPSF
Habari za Siasa

Rais Magufuli ‘aichoka’ TPSF

Spread the love

RAIS John Magufuli ameonesha kutofurahishwa na utendaji kazi wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), na kushauri kwamba, kama imeshindwa kutatua changamoto za wafanyabaishara, kianzishwe chombo kingine. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wake na wafanyabaishara zaidi ya 1,000 kutoka mikoa yote Rais Magufuli amhoji kwamba, je kuna sababu ya kuanzisha chombo kingine ambacho kitakuwa kiunganishi cha wafanyabiashara kwenye maeneo yao?

Rais Magufuli amehoji hayo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya wafanyabaishara kwamba, TPSF imekuwa jukwaa la kuwagandamiza wafanyabiashara wengi na kutengeneza kundi wanalolitaka wao.

“Wapo wengine na hili nataka nizungumze Bwana Shamte (Salum Shamte, Mwenyekiti TPSF) baadhi ya wafanyabaishara wamekuwa wakizungumza, inawezekana leo wakaogopa kuzungumza hapa wewe upo, wanasema TPSF imekuwa jukwaa la kuwagandamiza wafanyabaishara.

“…na kutengeneza ‘group’ (kundi) la watu fulani fulani wanaojiita wawakilishi wa wafanyabaishara mtayajibu ninyi wenyewe, mimi jukumu langu ni kusema,  je kuna sababu ya kuanzisha chombo kingine ambacho kitakuwa ‘direct link’ na watu wengine katika maeneo yao?”

Mbele ya Shamte,  Rais Magufuli amesema, yeye sio mnafiki na kwamba, panapohitajika kueleza ukweli, atafanya hivyo ili wahusika wajirekebishe.

 “Ukiwa msemaji wa wafanyabiashara lazima ujue biashara inaendeshwaje, najaribu kuyazungumza haya wenzangu mimi sio mnafiki. Mimi napasuaga hapo hapo, huku unaniangalia huku nalisema hivyo hivyo.

“Ili kusudi tufike mahali tujirekebishe,  ‘ku-formulate’ (kufanya) kitu ambacho kitawasemea ninyi wafanyabaishara,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!