Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema: Hatujui alipo Nyalandu
Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Hatujui alipo Nyalandu

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo Chadema), kimeeleza kutojua alipo Lazaro Nyalandu, aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya Awamu ya Nne. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Licha ya taarifa za kukamatwa kwake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, Tumaini Makene, msemaji wa chama hicho amesema, taarifa za tukio hilo zipo ofsini kwake na kwamba, mpaka sasa hawajui alipo.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, Nyalandu ambaye alikuwa kada wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Chadema Novemba 2017, alichukuliwa leo tarehe 26 Mei 2019 wakati akiwa kwenye kikao cha ndani cha chama hicho katika eneo la Itaja, Singida Kaskazini.

Makene amesema, wakati Nyalandu akiwa kwenye kikao hicho katika jimbo ambalo aliliongoza wakati akiwa CCM, walifika watu wenye silaha za moto waliojitamblisha kuwa ni askari, watu hao waliondoka na Nyalandu, David Jumbe na Mwenyekiti wa Chadema, Kata ya Itaja.

“Ni kweli mpaka sasa hatujui alipo, taarifa zilizopo mpaka sasa ni kwamba, watu hao waliofika eneo hilo na gari nyeupe, …walijitambulisha kuwa ni askari na walimuomba Nyalandu, Jumbe na mwenyekiti wa chama katika eneo hilo,” amesema Makene na kuongeza:

“Taarifa hizo ni kwamba, watu hao wakatoka nje na kuondoka nao. Hawakusema wanakwenda wapi. Naingia kwenye kikao kwa sasa, kama kuna zaidi nitumie ujumbe, nitakujibu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

error: Content is protected !!