Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uingereza atangaza kujiuzulu
Kimataifa

Waziri Mkuu Uingereza atangaza kujiuzulu

Theresa May, Waziri Mkuu wa Uingereza
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Theresa May ametangaza kujiuzulu wadhifa huo ifikapo tarehe 7 Juni 2019, kufuatia mkakati wake wa kuliondoa taifa hilo kwenye Umoja wa Ulaya (EU) kukwama. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

May ametangaza hayo leo tarehe 24 Mei 2019 akiwa mjini Downing Street, Uingereza.

Amesema, anajutia kitendo cha kukwama kwa mpango wake huo unaofahamika kama Brexit na kwamba, kwa maslahi ya taifa hilo, amejiuzulu ili lipate waziri mkuu mpya akiamini kwamba, ndiye atakayekuwa suluhu.

Kufuatia hatua hiyo, May ataendelea kushikilia wadhifa huo hadi pale mchakato wa upatikanaji wa waziri mkuu mpya utakapokamilika kwa kiongozi mpya kuchaguliwa.

Aidha, May amejiuzulu wadhifa wa uongozi wa chama cha Conservative na kwamba taachia ngazi rasmi tarehe 7 Juni 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!