Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uingereza atangaza kujiuzulu
Kimataifa

Waziri Mkuu Uingereza atangaza kujiuzulu

Theresa May, Waziri Mkuu wa Uingereza
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Theresa May ametangaza kujiuzulu wadhifa huo ifikapo tarehe 7 Juni 2019, kufuatia mkakati wake wa kuliondoa taifa hilo kwenye Umoja wa Ulaya (EU) kukwama. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

May ametangaza hayo leo tarehe 24 Mei 2019 akiwa mjini Downing Street, Uingereza.

Amesema, anajutia kitendo cha kukwama kwa mpango wake huo unaofahamika kama Brexit na kwamba, kwa maslahi ya taifa hilo, amejiuzulu ili lipate waziri mkuu mpya akiamini kwamba, ndiye atakayekuwa suluhu.

Kufuatia hatua hiyo, May ataendelea kushikilia wadhifa huo hadi pale mchakato wa upatikanaji wa waziri mkuu mpya utakapokamilika kwa kiongozi mpya kuchaguliwa.

Aidha, May amejiuzulu wadhifa wa uongozi wa chama cha Conservative na kwamba taachia ngazi rasmi tarehe 7 Juni 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!