Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM amfuata Rais Ramaphosa Afrika Kusini
Habari za SiasaTangulizi

JPM amfuata Rais Ramaphosa Afrika Kusini

Spread the love

RAIS John Magufuli anatarajiwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa zinazotarajiwa kufanyika kesho tarehe 25 Mei 2019. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa  tarehe 24 Mei 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, Rais Magufuli leo ameongozana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete kuelekea nchini Afrika Kusini kwa ajili ya kuhudhuria hafla hiyo.

Pia, katika safari hiyo Rais Magufuli ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula.

Aidha, taarifa ya Msigwa inaeleza kwamba baada ya Rais Magufuli kuhudhuria sherehe hiyo, anatarajia kufanya ziara rasmi ya kitaifa nchini Namibia ikiwemo kuzindua mtaa uliopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.

“Prof. Kabudi amesema baada ya kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Mteule Ramaphosa, Rais Magufuli atafanya ziara rasmi ya kitaifa nchini Namibia ambako pia atazindua mtaa ulipoewa jina la Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere kwa kutambua mchango mkubwa alioutoa katika ukombozi wa taifa hilo,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!