Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko DCI, Jeshi la Polisi lachunguza video inayodaiwa ya Mch. Gwajima
Habari Mchanganyiko

DCI, Jeshi la Polisi lachunguza video inayodaiwa ya Mch. Gwajima

Spread the love

JESHI la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limeanza uchunguzi wa video ya ngono, inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii inayodaiwa kuwa ni ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi, Kanda ya Dar es Salaam, Kamanda Lazaro Mambosasa wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 8 Mei 2019 jijini humo.

Kamanda Mambosasa amesema, Jeshi la Polisi la kanda hiyo kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), limeanza uchunguzi wa video hiyo.

Kamanda Mambosasa amesema, Askofu Gwajima sio mtuhumiwa wa usambazaji huo kama baadhi ya watu wanavyodhani na kwamba, ni muathirika wa tukio hilo, hivyo amewataka wananchi kuacha kusambaza video hiyo kwa kuwa ni kosa la jinai.

“Jeshi la Polisi limeanza uchunguzi wa video hiyo ya ngono mara moja na linapenda kuwataarifu wananchi kwamba Askofu Gwajima sio mtuhumiwa bali ni muathirika wa tukio hilo kwani jambo hili linaweza kufanywa na mtu yeyote kwa nia ya kumharibia heshima yake kwa jamii na waumini wake,” amesema Kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amewataka waumini wa Askofu Gwajima kuwa watulivu wakati uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea kufanywa na Jeshi la Polisi, ili kubaini aliyesambaza video hiyo na lengo la kufanya hivyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

error: Content is protected !!