Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Magufuli ateua mwenyekiti mpya TASAC
Habari Mchanganyiko

Rais Magufuli ateua mwenyekiti mpya TASAC

Rais John Magufuli
Spread the love

MKUU wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Profesa Tadeo Andrew Satta, ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC). Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa, uteuzi wa Prof. Satta umeanza jana tarehe 23 Aprili 2019.

Vile vile, Rais Magufuli ameteua Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TASAC, akiwemo Daniel Mchome, Mussa Mandia, Evelyne Makala, Renatus Mkinga, Japhet Massele na Bernard Asubisye.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Emmanuel Ndomba kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TASAC.
“Uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TASAC, Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TASAC na Mkurugenzi wa TASAC umeanza leo (jana) tarehe 23 Aprili 2019,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!