Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi, ACT-Wazalendo wavimbiana
Habari za Siasa

Polisi, ACT-Wazalendo wavimbiana

Spread the love

JESHI la Polisi nchini, limekataza kufanyika maandamano ya tarehe 9 Aprili 2019 yaliyopangwa na Ngome ya Vijana wa Chama cha ACT-Wazalendo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Wakati jeshi hilo likikataza maandamano hayo, ACT-Wazalendo wameeleza kuwa, watafanya kwa kuwa ni haki yao ya kikatiba.

Tarehe 6 Aprili 2019 Isack Nyasilu, Katibu wa Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo, alitangazakufanya maandamano kesho tarehe 9 Aprili, 2019 kupinga azimio la bunge la kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.

Taarifa hiyo ya zuio la polisi imewekwa leo tarehe 8 Aprili 2019 katika ukurasa wake wa Twitter wa ACT-Wazalendo ikieleza kuwa, polisi wamepiga marufuku maandamano hao.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto amezuia maandamano hayo.

Licha ya zuio hilo, Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo imesema, utaratibu wake katika kushiriki maandamano hayo uko pale pale.

“Tumepokea taarifa RPC wa Dodoma kuwa amezuia maandamano ya Ngome, Jumuiya na Mabaraza ya Vijana ya Vyama vya siasa.

“Tunapenda kumjulisha kuwa, sisi kama Social Auditors tunahaki ya kuhoji na kusimama na CAG, tunaendelea na maandamano kama yalivyopangwa kwa kuwa, ni haki yetu ya kikatiba,” inaeleza taarifa ya Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, utaratibu wa usafiri wa kutoka Dar es Salaam, Morogoro, Singida na Iringa kwenda Dodoma kushiriki maandamano ya tarehe 9/4/19 upo kama ulivyopangwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!