HAMIDU Bobali, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Lindi amesema kuwa, hatoacha ubunge na kujiunga ACT-Wazalendo alikohamia Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).
Amesema, hatofanya hivyo kwa sababu hatua hiyo inaweza kusababisha taifa kuingia kwenye hasara ya kurudia uchaguzi na kupoteza fedha nyingi lakini pia hawezi kujizulu kwani atakuwa amesaliti walimpigia kura wake.
Akizungmza leo tarehe 19 Machi 2019 Bobali amesema kuwa, hajabaki CUF kuungana na Prof. Lipumba ili kulinda ubunge wake, bali amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kulinda masilahi ya wapiga kura wake na kuokoa fedha za umma.
“…muda wa kwenda mahakamani haupo, tuachane na habari za kesi turudi kujenga chama chetu,” amesema Bobali nakuongeza; “Natoa rai kwa wabunge wenzangu, madiwani na wenyeviti tusikimbie chama chetu, tuje tujenge chama chetu.”
Katika hatua nyingine, Bobali ameomba radhi uongozi wa CUF na yeyote aliyemkosea ndani ya chama hicho. “Na leo ninautangazia umma na chama, nikiwa mbunge na mwanachama naamini yule niliyomkosea, mwenyekiti atakuwa amenisamehe. Ninachukua fursa hii kuomba radhi wanachama wote na viongozi wa CUF ambao kwa namna moja au nyingine tumekosena.’
Leave a comment