Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kinachonibakisha CUF si Prof. Lipumba-Mbunge CUF
Habari za Siasa

Kinachonibakisha CUF si Prof. Lipumba-Mbunge CUF

Hamidu Bobali, Mbunge wa Mchinga
Spread the love

HAMIDU Bobali, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Lindi amesema kuwa, hatoacha ubunge na kujiunga ACT-Wazalendo alikohamia Maalim Seif Sharif Hamad, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CUF. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Amesema, hatofanya hivyo kwa sababu hatua hiyo inaweza kusababisha taifa kuingia kwenye hasara ya kurudia uchaguzi na kupoteza fedha nyingi lakini pia hawezi kujizulu kwani atakuwa amesaliti walimpigia kura wake.

Akizungmza leo tarehe 19 Machi 2019 Bobali amesema kuwa, hajabaki CUF kuungana na Prof. Lipumba ili kulinda ubunge wake, bali amechukua hatua hiyo kwa ajili ya kulinda masilahi ya wapiga kura wake na kuokoa fedha za umma.

“…muda wa kwenda mahakamani haupo, tuachane na habari za kesi turudi kujenga chama chetu,” amesema Bobali nakuongeza; “Natoa rai kwa wabunge wenzangu, madiwani na wenyeviti tusikimbie chama chetu, tuje tujenge chama chetu.”

Katika hatua nyingine, Bobali ameomba radhi uongozi wa CUF na yeyote aliyemkosea ndani ya chama hicho. “Na leo ninautangazia umma na chama, nikiwa mbunge na mwanachama naamini yule niliyomkosea, mwenyekiti atakuwa amenisamehe. Ninachukua fursa hii kuomba radhi wanachama wote na viongozi wa CUF ambao kwa namna moja au nyingine tumekosena.’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!