Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Zitto siyo mnafiki kama yule
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Zitto siyo mnafiki kama yule

Spread the love

MAALIM Seif Shariff Hamad, mwanachama mpya wa Chama cha ACT-Wazalendo, amemweleza Zitto Kabwe kwamba sio mnafiki. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Akikaribishwa Makao Makuu ya ACT-Wazalendo Kijitonyama jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Machi 2019 Maalim Seif, ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa CUF amesema, uamuzi wa kujiunga na ACT-Wazalendo umesukumwa na mambo mengi ikiwemo uimara wa chama hicho na viongozi wake

“Zitto sio mnafiki kama yule (hakumtaja jina). Sio aina ya viongozi anayejikomba kwa wakubwa,” amesema Maalim Seif.

Kwenye mkutano huo uliotumika kumkabidhi kadi ya uanachama wa ACT- Wazalendo Maalim Seif amesema, chama hicho kina viongozi wenye ujasiri, adabu na wanaoendana na mazingira.

Akimwelezea Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa chama hicho amesema, sio kiongozi muoga jambo linalomfanya kuwa kiongozi imara kwa zama hizi.

“Zitto ni mtu makini, ni kiongozi ambaye hasemi jambo bila kufanya utafiti na pale anapomaliza utafiti wake hutoa matamko bila woga wowote,” amesema.

Ameeleza kuwa, kabla ya kufanya uamuzi wa kujiunga na ACT-Wazalendo, walifanya utafiti kwa vyama vine.

“Tulifanya utafiti Chadema, NLD, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo, tukajiridhisha na kufanya uamuzi wa kuhamia ACT- Wazalendo,” amesema.

Amefafanua kuwa, vyama vyote walivyopita kubisha hodi ili wapokewe vina ubora lakini ACT-Wazalendo waliona ndio kinachowafaa zaidi.

Maalim Seif amejiunga na ACT-Wazalendo jana terehe 18 Machi 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!