Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif: Zitto siyo mnafiki kama yule
Habari za SiasaTangulizi

Maalim Seif: Zitto siyo mnafiki kama yule

Spread the love

MAALIM Seif Shariff Hamad, mwanachama mpya wa Chama cha ACT-Wazalendo, amemweleza Zitto Kabwe kwamba sio mnafiki. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Akikaribishwa Makao Makuu ya ACT-Wazalendo Kijitonyama jijini Dar es Salaam leo tarehe 19 Machi 2019 Maalim Seif, ambaye alikuwa Katibu Mkuu wa CUF amesema, uamuzi wa kujiunga na ACT-Wazalendo umesukumwa na mambo mengi ikiwemo uimara wa chama hicho na viongozi wake

“Zitto sio mnafiki kama yule (hakumtaja jina). Sio aina ya viongozi anayejikomba kwa wakubwa,” amesema Maalim Seif.

Kwenye mkutano huo uliotumika kumkabidhi kadi ya uanachama wa ACT- Wazalendo Maalim Seif amesema, chama hicho kina viongozi wenye ujasiri, adabu na wanaoendana na mazingira.

Akimwelezea Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa chama hicho amesema, sio kiongozi muoga jambo linalomfanya kuwa kiongozi imara kwa zama hizi.

“Zitto ni mtu makini, ni kiongozi ambaye hasemi jambo bila kufanya utafiti na pale anapomaliza utafiti wake hutoa matamko bila woga wowote,” amesema.

Ameeleza kuwa, kabla ya kufanya uamuzi wa kujiunga na ACT-Wazalendo, walifanya utafiti kwa vyama vine.

“Tulifanya utafiti Chadema, NLD, NCCR-Mageuzi na ACT-Wazalendo, tukajiridhisha na kufanya uamuzi wa kuhamia ACT- Wazalendo,” amesema.

Amefafanua kuwa, vyama vyote walivyopita kubisha hodi ili wapokewe vina ubora lakini ACT-Wazalendo waliona ndio kinachowafaa zaidi.

Maalim Seif amejiunga na ACT-Wazalendo jana terehe 18 Machi 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!