Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Kwanini twende ACT Wazalendo na sio Chadema?
Makala & Uchambuzi

Kwanini twende ACT Wazalendo na sio Chadema?

Spread the love

MAHAKAMA Kuu ya Tanzania kupitia Jaji Benhajj Masoud, imeamua kumhalalisha Lipumba (Pro. Ibrahim Lipumba) kama mwenyekiti halali wa CUF.

Sisi tumeendelea kusimamia msimamo wetu kwamba, hatuwezi kufanyakazi na Lipumba na kwa sababu ambazo tumekuwa tukizisema mara kadhaa na ambazo umma umekuwa ukizua kwa mapana yake.

Lakini swali kubwa au hofu kubwa kutoka kwa umma ambao umekuwa unatuunga mkono umekuwa ukituamini kujua tutakwenda wapi.

Na kama tutajiunga na chama tutajiunga na chama gani? Na vyama viwili vikipewa nguvu kubwa zaidi ni ACT-Wazalendo na Chadema na wamekuwepo watu wakitamani tujiunge Chadema.

Kwanza niseme tu, maoni yote ni sahihi kabisa, lakini sisi kama watu ambao nyuma yetu kuna umma mkubwa na tukizingatia sababu za kukataa kufanyakazi na Lipumba pamoja na dhamira ovu ya dola yetu, tuna kila sababu za kufanya uchaguzi sahihi.

Tukijiunga Chadema, maana yake ni kwamba, tutakuwa na chama kimoja cha upinzani chenye nguvu, Bara na Zanzibar na sio viwili au vitatu tena. Maana lengo la adui tangu mwanzo ni kuhakikisha anaua nguvu za upinzani, na haswa vyama viwili Chadema na CUF.

 Na ameshafanikiwa kukiua CUF hivyo kimebaki chama kimoja jambo ambalo kwake anaweza kuwa na fursa kubwa zaidi ya kushughulika na chama kimoja tofauti na mwanzo alipokuwa anashughulika na vyama viwili. Adui yetu atakuwa amefanikiwa.

Tukihamia ACT-Wazalendo ni kweli kwamba, ACT itakuwa chama kipya chenye nguvu kuliko wakati wowote ule. Na hivyo kufanya upinzani kuwa kwenye nafasi nzuri zaidi na nguvu zaidi.

Kwamba, ACT ambacho kitakuwa na mtaji mkubwa Zanzibar na Bara pia, kitakuwa kwenye nafasi nzuri ya kufanya siasa na kuimarisha upinzani kwasababu nguvu ileile ya upinzani iliyokuwepo kabla kutokana na uwepo wa vyama viwili vya upinzani Chadema na ACT Wazalendo, havina migogoro ya ndani na vinakuwa kwenye nafasi ya kufanya siasa kikamilifu.

Hivyo lengo la Magufuli kuviua vyama vya upinzani litakuwa limeviimarisha zaidi vyama hivi kuliko wakati mwingine. Watu walewale ambao miaka takrabani miwili tumekuwa kwenye mgogoro usio kwisha, sasa tunakwenda kufanya siasa kimamilifu.

Makala haya imechukuliwa kutoka mitandao

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

error: Content is protected !!