Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba atwaa uenyekiti CUF
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba atwaa uenyekiti CUF

Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba ametwaa nafasi ya uenyekiti wa chama hicho kwa mara nyingine. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Miongoni mwa majukumu ya leo katika Mkutano Mkuu wa CUF ni pamoja na kupata viongozi mbalimbali wa chama hicho.

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi huo uliofanyika leo tarehe 12 Machi 2019, Thenei Juna Ally amesema, Prof. Lipumba amepata jumla ya kura 516 ikiwa ni zaidi ya asilimia 88 ya kura zote.

Thenei amemtangaza pia Maftaha Nachuma kuwa ameshinda nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara kwa kupata kura 231 sawa na asilimia 40 huku Makamu Mwenyekiti Visiwani akitajwa kuwa Abas Juma Muhunzi ambaye alipata kura 349 sawa na asilimia 60.9.

Prof. Lipumba baada ya kutangazwa kushinda amesema, walioshinda katika nafasi nyingine ni vijana wake na kwmaba, atakwenda nao vizuri katika kuongoza chama hicho.

Mkutano Mkuu wa chama hicho ulianza jana na untarajiwa kumalizika kesho tarehe 14 Machi 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!