Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa UVCCM wamnanga Lowassa
Habari za SiasaTangulizi

UVCCM wamnanga Lowassa

Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu
Spread the love

WAKATI wengine wakimtete Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea urais kupitia Chadema kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 na kuamua kuhamia CCM tarehe 1 Machi 2019, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) waanza kumsigina. Anaripoti Dany Tibason…(endelea).

UVCCM imempokea Lowassa, aliyewahi kuwa Waziri Mkuu lakini imempa masharti kwamba, akae kimya kuzingatia, kutafakari na kuyaishi matakwa ya chama hicho na si vinginevyo.

Umoja huo umeeleza kuwa, kurejea kwa Lowassa hakuwezi kutafsiriwa kuwa ni dhambi ila kinachotakiwa ni kukaa kimya ili aendelee kuwa mwanachama wa chama hicho baada ya kupokewa.

Mbali na hilo UVCCM wameeleza kwamba, Lowassa hakuombwa kurejea CCM bali yeye mwenyewe na ndiye aliyeomba na kwamba, taratibu za kumfikiria na kumjadili zilifanywa ikiwa ni pamoja na kumtaka kujieleza na kukiri makosa aliyoyafanya akiwa mwanachama wa CCM.

Khery James, Mwenyekiti wa UVCCM akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 11 Machi 2019 jijini Dodoma amesema, kwa sasa Lowassa anachukuliwa kama mwanachama mpya ndani ya chama hicho na ndiyo maana alipewa kadi mpya na siyo ile ya zamamni aliyokuwa akiimiliki.

Amesema, Lowassa pamoja na kurejea CCM lakini ni lazima akubali kusikiliza kile ambacho kinatakiwa ndani ya chama kwa kufuata misingi, kanuni na taratibu ndani za chama husika na si viginevyo.

Amesema, CCM ina maadili yake na si chama ambacho mtu anaweza kuingia na kujichukulia uamuzi wake mwenyewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!