Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Michezo Mchezaji Yanga afungiwa mechi tatu
Michezo

Mchezaji Yanga afungiwa mechi tatu

Clifford Ndimbo, Msemaji wa TFF
Spread the love

BEKI wa klabu ya Yanga Abdallah Shaibu ‘Ninja’ amefungiwa michezo mitatu baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga kiwiko mchezaji Andrew Simchimba kwenye mchezo dhidi Coastal Union uliochezwa 3 februari, 2019. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea)

Mchezaji huyo ambae alihojiwa na kamati ya nidhamu hapo jana alikili kosa hilo na kusema haikuwa dhamila yake bali alikuwa akijaribu kumzuia asipite hivyo kamati ikaamua kumsimamisha michezo mitatu mfululizo.

Afisa Habari wa shirikisho la mpira Tanzania TFF Clifford Ndimbo ameeleza kuwa Kamati hiyo ambayo ilikutana  jana jumapili chini ya mwenyekiti wake wakili Kiomoni Kibamba.

“Kamati imempa adhabu ya kufungiwa kutocheza michezo mitatu mfululizo kwa mujibu wa kifungu cha 48(1) (d) cha kanuni ya nidhamu” alisema Ndimbo

Hapo awali mcherzaji huyo aliitwa na kamati ya nidhamu ya shirikisho la mpira wa miguu nchini Tff na kushindwa kutokea kutokana na timu yake kuwa katika michezo mikoani.

Ninja ambae kwa sasa amekuwa mchezaji muhimu kwenye kikosi cha Yanga ataikosa michezo dhidi ya Lipuli Fc, Ndanda na African Lyon.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Vijana waadhimisha miaka 62 ya Uhuru kwa kushiriki michezo

Spread the loveUMOJA wa Vijana wa CCM (UVCCM) tawi la Mlowo, jana...

Michezo

Pesa ipo huku Meridianbet, beti sasa

Spread the love  WIKIENDI inaishia leo hii jaman kama bado hujasuka mkeka...

Michezo

Wenzako wameshakuwa mamilionea hapa wewe unasubiri nini?

Spread the love  WIKIENDI imefika na ukiachana na mvua za Dar es...

Michezo

Manchester City vichwa chini Ligi Kuu England

Spread the love MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Uingereza klabu yaManchester City...

error: Content is protected !!