Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Serengeti Boys kujiuliza kwa Australia
Michezo

Serengeti Boys kujiuliza kwa Australia

Kikosi cha Serengeti Boys wakiwa katika mazoezi mepesi wakijiandaa na mchezo wao dhidi ya Australia
Spread the love

BAADA ya kupoteza kwa bao 1-0 mbele ya Guinea kwenye mchezo wa kwanza wa kundi A, timu ya taifa ya vijana Serengeti Boys itajiuliza tena mbele ya Australia kwenye mchezo wao wa pili utakaochezwa juni 6, 2019 kwenye michuano ya ya UEFA assist. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Goli pekee la Guinea kwenye mchezo huo lilifungwa na Conte Osky kwenye kipindi cha kwanza ambalo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo nakufanikiwa kuondoka na alama tatu.

Baada ya mchezo huo kukamilika kocha mkuu wa Serengeti Boys, Oscra Mirambo alisema kuwa timu haikuwa vizuri kipindi cha kwanza lakini tulikuwa bora sana kipindi cha pili baada ya kufanya marekebisho na alitumia mchezo huo kama kipimo.

“Tuna amini huu mchezo ulikuwa ni kipimo kizuri licha ya mazingira kutubana, kama uwanja kujaa maji lakini mwisho wa siku kuna vitu vingi chanya ambavyo tumevichukua kutoka kwenye mechi hii lakini bado kuna changamoto nazotakiwa kutatua,” alisema kocha huyo.

Mchezo unaofuata wa Serengeti Boys itakuwa Machi 6 dhidi ya Australia na kumaliza mechi ya mwisho kwenye kundi hilo dhidi ya mwenyeji Uturuki Machi 8.

Timu hiyo ambayo ipo nchini Uturuki kwenye michuano hiyo ambayo imeandaliwa na kusimamiwa na Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA) inatakiwa kushinda michezo hiyo miwili iliyobaki ili iweze kufuzu kwenye hatua ya robo fainali.

Timu hiyo imekwenda kushiriki michuano hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa COSAFA 2018 nchini Botswana na kupata mwaliko wa kwenda kushiriki michuano ya UEFA assist inayoaandaliwa na shirikisho la mpira wa miguu barani ulaya (UEFA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!