Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo IFAB yafanya mabadiliko ya kanuni kwenye Soka
Michezo

IFAB yafanya mabadiliko ya kanuni kwenye Soka

Mpira wa miguu
Spread the love

BODI ya Kimataifa ya Shirikisho la Mpira wa Miguu (IFAB) imefanya mabadiliko ya kanuni ya mchezo wa soka kwenye kikao kilichofanyika wiki iliyopita nchini Scotland na mabadiliko hayo yataanza kutumika misimu ujao wa mashindano 2019/20. Inalipoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

IFAB imefanya jumla ya mabadiliko saba yakihusisha sehemu ya ndani ya uwanja na nje ya uwanja wakati mchezo husika ukiendelea.

Badiliko la kwanza ni kutokuwa na mrejesho (rebound) kwenye pigo la penalti na mchezo utasimama kwa kuanzishwa kama mpira wa penalti utakuwa umeokolewa au kugonga mwamba kwa hiyo hakutokuwa na haja ya wachezaji kujipanga nje ya boksi wakati penalti hiyo ikipigwa.

Badiliko la pili, endapo goli lolote litafungwa likiwa limegusa mkono wa mchezaji kwa makusudi au bahati mbaya halitakubalika na endapo mchezaji atakuwa anafanyiwa mabadiliko ataruhusiwa kutoka kupitia upande wowote ule wa uwanja ili kuepusha swala la kupoteza muda.

Mabadiliko mengine yaliofanywa na bodi hiyo ni mpira wa kuanza kwa kipa (goal kick) mchezaji ataruhusiwa kuugusa mpira huo hata akiwa ndani ya eneo la boksi kutoka kwa kipa tofauti na hapo awali mchezaji alikuwa haruhusiwi kugusa mpira huo mpaka utoke nje ya boksi.

Kwa upande wa makocha nao watakuwa wanaoneshwa kadi ya njano na nyekundu tofauti na sasa wanaambiwa watoke tu kwenye eneo la benchi la ufundi na baada ya kuoneshewa kadi hiyo nao watakuwa wanakosa baadhi ya michezo.

Maeneo mengine yaliofanyiwa mabadiliko ni kwenye kuweka ukuta wa kuzuia mpira wa adhabu ndogo (foul) ambapo wachezaji wa wanapiga mpira huo hawatoruhusiwa kwenda kujumuika kwenye ukuta wa timu ambayo inazuia mpira huo, na kwenye adhabu kubwa ya penalti makipa wataruhusiwa kuweka mguu mmoja kwenye mstari na mwingine kuamua ukae popote.

Hivi karibuni mchezo wa mpira wa miguu umekuwa ukifanyiwa mabadiliko mengi ikiwamo ya teknolojia kama kutumia video katika maamuzi (video assistance referee) iliyotumika kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya kombe la Dunia iliyofanyika Urusi Juni, 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!