Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Michezo Serengeti Boys kujiuliza kwa Australia
Michezo

Serengeti Boys kujiuliza kwa Australia

Kikosi cha Serengeti Boys wakiwa katika mazoezi mepesi wakijiandaa na mchezo wao dhidi ya Australia
Spread the love

BAADA ya kupoteza kwa bao 1-0 mbele ya Guinea kwenye mchezo wa kwanza wa kundi A, timu ya taifa ya vijana Serengeti Boys itajiuliza tena mbele ya Australia kwenye mchezo wao wa pili utakaochezwa juni 6, 2019 kwenye michuano ya ya UEFA assist. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Goli pekee la Guinea kwenye mchezo huo lilifungwa na Conte Osky kwenye kipindi cha kwanza ambalo lilidumu mpaka mwisho wa mchezo nakufanikiwa kuondoka na alama tatu.

Baada ya mchezo huo kukamilika kocha mkuu wa Serengeti Boys, Oscra Mirambo alisema kuwa timu haikuwa vizuri kipindi cha kwanza lakini tulikuwa bora sana kipindi cha pili baada ya kufanya marekebisho na alitumia mchezo huo kama kipimo.

“Tuna amini huu mchezo ulikuwa ni kipimo kizuri licha ya mazingira kutubana, kama uwanja kujaa maji lakini mwisho wa siku kuna vitu vingi chanya ambavyo tumevichukua kutoka kwenye mechi hii lakini bado kuna changamoto nazotakiwa kutatua,” alisema kocha huyo.

Mchezo unaofuata wa Serengeti Boys itakuwa Machi 6 dhidi ya Australia na kumaliza mechi ya mwisho kwenye kundi hilo dhidi ya mwenyeji Uturuki Machi 8.

Timu hiyo ambayo ipo nchini Uturuki kwenye michuano hiyo ambayo imeandaliwa na kusimamiwa na Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA) inatakiwa kushinda michezo hiyo miwili iliyobaki ili iweze kufuzu kwenye hatua ya robo fainali.

Timu hiyo imekwenda kushiriki michuano hiyo baada ya kutwaa ubingwa wa COSAFA 2018 nchini Botswana na kupata mwaliko wa kwenda kushiriki michuano ya UEFA assist inayoaandaliwa na shirikisho la mpira wa miguu barani ulaya (UEFA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

BiasharaMichezo

Piga pesa kupitia Derby ya London Kaskazini kwa kubadhiri na Meridianbet

Spread the love NAJUA umesikia na unazijua Derby nyingi kutoka jiji la London,...

error: Content is protected !!